Radio Tambua

UTAMBUZI: Suluhisho la kukumbana na udanganyifu

Danson Ottawa

Use Left/Right to seek, Home/End to jump to start or end. Hold shift to jump forward or backward.

0:00 | 23:43

Mahubiri haya yanaangazia onyo la Mtume Paulo dhidi ya walimu wa uongo katika 2 Kor. 11. Paulo anashangazwa na jinsi Wakorintho wanavyoondoka haraka kutoka kwa ibada ya kweli kwa Kristo, wakivutwa na mitume wa uongo wanaomuubiri Yesu mwingine, injili nyingine, na roho mwingine. Katika mahubiri hayo, Danson Ottawa anaangazia hatari ya sasa ya udanganyifu na kumtia moyo msikilizaji kufuatilia utambuzi wa Biblia. Anasema, “Waumini waliowekwa msingi katika kweli, na kukua katika neema, wataweza kuilinda Injili”.